Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi Idrissa Kitwana Mustafa amewataka Masheha wa Mkoa huo kuongeza mashirikiano katika utendaji wa kazi zao.
![](http://mjinimagharibi.go.tz/wp-content/uploads/2022/11/1029SALAH-1024x683.jpg)
Amesema mashirikiano baina yao ndio njia pekee itakayoweza kuleta ufanisi katika kuwahudumia wananchi pamoja na kufanikisha masuala mbali mbali ya Serikali yanayotekelezwa ndani ya Shehia zao.
![](http://mjinimagharibi.go.tz/wp-content/uploads/2022/11/957SALAH-1024x683.jpg)
Mkuu wa Mkoa amesema hayo mara baada ya kuwaapisha masheha wapya aliyowateua hivi karibuni katika Shehia kadhaa za Mkoa huo.
![](http://mjinimagharibi.go.tz/wp-content/uploads/2022/11/955SALAH-1024x683.jpg)
Naye Mkuu wa Wilaya ya Magharibi “A” Suzan Kunambi amesema kazi ya Masheha ni kuwahudumia wananchi hivyo amewataka kutimiza wajibu wao kikamilifu.
![](http://mjinimagharibi.go.tz/wp-content/uploads/2022/11/1009SALAH-1024x683.jpg)
Amesema yapo mambo ambayo Masheha wangeweza kuyafanyia kazi na kuyapatia ufumbuzi badala ya kuwaelekeza Wananchi kuyapeleka ngazi ya Wilaya na Mkoa.
![](http://mjinimagharibi.go.tz/wp-content/uploads/2022/11/970SALAH-1024x683.jpg)
Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa Mjini Magharibi Moh’d Ali Abdalla amewahimiza Masheha kufanya kazi kwa kufuata Sheria katika kutekeleza wajibu wao.
![](http://mjinimagharibi.go.tz/wp-content/uploads/2022/11/994SALAH-1024x683.jpg)
Masheha waliyoapishwa ni Mohammed Mussa Machano Shehia ya Kwahani, Omar Juma Masoud Shehia ya Kihinani na Khamis Bakari Juma Shehia ya Kama.
![](http://mjinimagharibi.go.tz/wp-content/uploads/2022/11/1041SALAH-1024x683.jpg)