Mwenge wa Uhuru umeanza mbio zake katika Mkoa Mjini Magharibi ukitokea Mkoa wa Dar-es-salaam.
![](http://mjinimagharibi.go.tz/wp-content/uploads/2023/05/WhatsApp-Image-2023-05-29-at-10.57.17-1-1024x683.jpeg)
Mapokezi ya Mwenge wa Uhuru yalifanyika katika Uwanja wa Ndege wa Abeid Amani Karume ambapo Mkuu wa Mkoa Dar-es-salam Albert Chalamila aliukabidhi Mwenge wa Uhuru kwa Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Idrissa Kitwana Mustafa.
![](http://mjinimagharibi.go.tz/wp-content/uploads/2023/05/WhatsApp-Image-2023-05-29-at-10.57.17-1024x683.jpeg)
Mara baada ya makabidhiano hayo, Mkuu wa Mkoa aliukabidhi Mwenge wa Uhuru kwa Mkuu wa Wilaya ya Mjini Rashid Simai Msaraka ili kuanza mbio zake katika Wilaya hiyo.
![](http://mjinimagharibi.go.tz/wp-content/uploads/2023/05/WhatsApp-Image-2023-05-29-at-10.57.16-1024x683.jpeg)
Jumla ya miradi 21 yenye dhamani ya zaidi ya shilingi bilioni 118 itapitiwa na Mwenge wa Uhuru katika Wilaya tatu za Mkoa Mjini Magharibi.
![](http://mjinimagharibi.go.tz/wp-content/uploads/2023/05/WhatsApp-Image-2023-05-29-at-10.59.45-1024x682.jpeg)
Mwenge wa Uhuru utaendelea na mbio zake kesho Jumanne katika Wilaya ya Magharibi ‘A’, siku ya Jumatano katika Wilaya ya Magharibi ‘B’ na Alkhamis tarehe 1 Juni utakabidhiwa Mkoa wa Kusini Unguja.
![](http://mjinimagharibi.go.tz/wp-content/uploads/2023/05/WhatsApp-Image-2023-05-29-at-10.57.15-1024x683.jpeg)